Na Princess Asia, Dar es Salaam
MBEYA City imepangwa kundi B katika michuano maalumu ijulikanayo kama Nile Basin itakayopigwa Sudan kuanzia Mei 22 hadi Juni 2.
Katika droo ya michuano hiyo inayoshirikisha washindi wa pili na mabingwa wa Kombe la FA wa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), iliyopangwa leo, Mbeya City iliyopewa nafasi ya Azam iliyojitoa imepangwa Kundi B pamoja na timu za AFC Leopards ya Kenya), El Merreikh Al Fasher ya Sudan na Elman ya Somalia.
Kundi A lina na timu za El Merreikh ya Sudan,
Victoria University ya Uganda, Malakia ya Sudan
Kusini na Polisi ya Zanzibar, wakati Kundi C linaundwa na Al Ahli Shandi ya Sudan, Al Masry ya Misri, Defence ya Ethiopia na Dkhill ya Djibouti na
Kundi D lina timu za Hey Al Arab ya Sudan, Arab
Contractors ya Misri, Flambeau ya Burundi na Etincelles ya Rwanda.
Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi amezungumzia droo hiyo na kusema wamepangwa kundi gumu, lakini watajipanga ili waweze kufanya vizuri. Amesema anafurahi ratiba wameipata mapema, itawasaidia kujipanga mapema.
MBEYA City imepangwa kundi B katika michuano maalumu ijulikanayo kama Nile Basin itakayopigwa Sudan kuanzia Mei 22 hadi Juni 2.
Katika droo ya michuano hiyo inayoshirikisha washindi wa pili na mabingwa wa Kombe la FA wa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), iliyopangwa leo, Mbeya City iliyopewa nafasi ya Azam iliyojitoa imepangwa Kundi B pamoja na timu za AFC Leopards ya Kenya), El Merreikh Al Fasher ya Sudan na Elman ya Somalia.
![]() |
Kikosi cha Mbeya City ambacho kitashiriki michuano mipya ya CECAFA |
Kundi A lina na timu za El Merreikh ya Sudan,
Victoria University ya Uganda, Malakia ya Sudan
Kusini na Polisi ya Zanzibar, wakati Kundi C linaundwa na Al Ahli Shandi ya Sudan, Al Masry ya Misri, Defence ya Ethiopia na Dkhill ya Djibouti na
Kundi D lina timu za Hey Al Arab ya Sudan, Arab
Contractors ya Misri, Flambeau ya Burundi na Etincelles ya Rwanda.
Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi amezungumzia droo hiyo na kusema wamepangwa kundi gumu, lakini watajipanga ili waweze kufanya vizuri. Amesema anafurahi ratiba wameipata mapema, itawasaidia kujipanga mapema.
0 comments:
Post a Comment