// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); RONALDO NA NYOTA ANAYEWATOA UDENDA MAN UNITED WAITWA URENO KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE RONALDO NA NYOTA ANAYEWATOA UDENDA MAN UNITED WAITWA URENO KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, May 13, 2014

    RONALDO NA NYOTA ANAYEWATOA UDENDA MAN UNITED WAITWA URENO KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA

    MCHEZAJI anayetakiwa na Manchester United, William Carvalho ameorodheshwa katika kikosi cha awali cha Ureno cha wachezaji 30 kwa ajili ya Kombe la Dunia sambamba na Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo.
    Kiungo huyo wa Sporting, ambaye anaweza kutua Old Trafford msimu ujao kama United wataendelea na nia ya kumsajili, aliichezea Ureno kwa mara ya kwanza katika mechi ya mwisho ya mchujo kuwania tiketi ya Brazil dhidi ya Sweden Novemba mwaka jana.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 atakuwa pamoja kwenye kikosi hicho na mchezaji wa Mashetani Wekundu hao, Luis Nani.
    Kama kawaida: Cristiano Ronaldo ataiongoza Ureno katika Kombe la DuniaSelected: Man United target William Carvalho (left) has been named in Portugal's provisional World Cup squad
    Ameteuliwa: William Carvalho (kushoto) anayetakiwa na Man United ameitwa kikosi cha Ureno

    KIKOSI CHA AWALI CHA URENO HIKI HAPA;

    MAKIPA: Anthony Lopes (Lyon), Beto (Sevilla), Eduardo (Braga), Rui Patricio (Sporting Lisbon)
    MABEKI: Andre Almeida (Benfica), Antunes (Malaga), Bruno Alves (Fenerbahce), Fabio Coentrao (Real Madrid), Joao Pereira (Valencia), Neto (Zenit), Pepe (Real Madrid), Ricardo Costa (Valencia), Rolando (Inter Milan)
    VIUNGO: Andre Gomes (Benfica), Joao Mario (Vitoria), Joao Moutinho (Monaco), Miguel Veloso (Dynamo Kiev), Raul Meireles (Fenerbahce), Ruben Amorim (Benfica), William Carvalho (Sporting Lisbon)
    WASHAMBULIAJI: Cristiano Ronaldo (Real Madrid), Eder (Braga), Helder Postiga (Lazio), Hugo Almeida (Besiktas), Ivan Cavaleiro (Benfica), Nani (Manchester United), Rafa (Braga), Ricardo Quaresma (Porto), Varela (Porto), Vieirinha (Wolfsburg).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO NA NYOTA ANAYEWATOA UDENDA MAN UNITED WAITWA URENO KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top