WENYEJI, Marekani wameibuka na ushindi wa kishindo wa mabao 4-1 dhidi ya Paraguay katika mchezo wa Kundi D Fainali za Kombe la Dunia Alfajiri ya leo Uwanja wa SoFi Jijini Inglewood, Los Angeles County, California.
Mabao ya USA yamefungwa na kiungo wa Sao Paulo ya Brazil, Damián Josué Bobadilla Benítez aliyejifunga dakika ya saba, mshambuliaji wa Monaco ya Ufaransa, Folarin Jerry Balogun aliyefunga mawili dakika ya 31 na 45’+5 na kiungo mshambuliaji wa Borussia Mönchengladbach ya Ujerumani, Giovanni Alejandro Reyna dakika ya 90’+8.
Bao pekee na la kufutia machozi la Paraguay katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Mholanzi, Danny Makkelie mbele ya mashabiki 70,492 limefungwa na kiungo wa Palmeiras ya Italia, Maurício Magalhaes Prado dakika ya 73.
Mchezo mwingine wa Kundi C utafuatia Saa 1:00 Asubuhi ya kesho kati ya Australia na Uturuki Uwanja wa BC Place Jijini Vancouver nchini Canada.



.png)
0 comments:
Post a Comment