// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); NIGERIA WAWASILI USIKU WA MANANE KUIVAA NGORONGORO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE NIGERIA WAWASILI USIKU WA MANANE KUIVAA NGORONGORO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, May 08, 2014

    NIGERIA WAWASILI USIKU WA MANANE KUIVAA NGORONGORO

    Na Prince Akbar, Dar es Salaam
    TIMU ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Nigeria, Flying Eagles imewasili usiku wa manane jana nchini tayari kwa mchezo dhidi ya Tanzania, Ngorongoro Heroes Jumapili hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwania tiketi ya Fainali za Afrika mwakani nchini Senegal.
    Eagles imewasili na msafara wa watu 30, wakiwemo wachezaji 18, miongoni mwao wanacheza Ulaya na kufikia katika hoteli ya kimataifa ya Sapphire Court, iliyopo makutano ya mitaa ya Lindi na Sikukuu, Dar es Salaam.
    Mkurugenzi wa Sapphire Court, Abdulfatah Salim Saleh ameiambia BIN ZUBEIRY Flying Eagles wamefika salama na kupatiwa huduma nzuri tayari kwa mchezo wa mwishoni mwa wiki.   
    Manu Garba, kocha wa Flying Eagles
    Flying Eagles kwa sasa inafundishwa na kocha aliyeipa Nigeria Kombe la nne la Dunia la U-17 mwaka jana, katika mashindano yaliyofanyika Falme za Kiarabu, Manu Garba.
    Garba ni kocha mwenye mafanikio Nigeria akiwa amewahi kuwa Msaidizi wa Yemi Tella wakati Golden Eaglets inatwaa taji la U17 Afrika mwaka 2007 mjini Lome, Togo kabla ya kutwaa na Kombe la Dunia pia nchini Korea.
    Aliiongoza pia timu ya jimbo la nyumbani kwao, Gombe Youth Team kutwaa ubingwa wa michuano ya U-18 ya Umbro mjini Manchester mwaka 2005.
    Mwanasoka huyo wa zamani wa kimataifa wa Nigeria, enzi zake alichezea klabu za El-Kanemi Warriors (1987-1993); Kano Pillars (1994); Gombe United (1995) na BCC Lions (1996).

    Alianza ukocha mara tu baada ya kustaafu kama mwalimu Msaidizi Gombe United kuanzia 1997 hadi 2008 kabla ya kuwa Mshauri wa Ufundi mwaka 2012.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NIGERIA WAWASILI USIKU WA MANANE KUIVAA NGORONGORO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top