// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MTANZANIA ANAYECHEZA UJERUMANI AOMBA KUZIPA PENGO LA SAMATTA TAIFA STARS - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MTANZANIA ANAYECHEZA UJERUMANI AOMBA KUZIPA PENGO LA SAMATTA TAIFA STARS - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, May 07, 2014

    MTANZANIA ANAYECHEZA UJERUMANI AOMBA KUZIPA PENGO LA SAMATTA TAIFA STARS

    Na Renatus Mahima, Dar es Salaam
    KINDA anayecheza soka ya kulipwa Ujerumani, Charles Mishetto ameomba kuitwa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars aisaidie katika kampeni za kuing’oa Zimbabwe.
    Hatua hiyo inakuja baada ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kuikubalia TP Mazembe ya DRC ambayo imegoma kuwaachia Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu kuitumikia Taifa Stars katika mechi ya kuwania kushiriki fainali zijazo za Afrika (AFCON) dhidi ya Zimbabwe.
    FIFA imesema klabu hazitashurutishwa kuwaachilia wachezaji wao ili washiriki mechi za kufuzu kwa michuano hiyo itakayofanyika Morocco mwakani, kwa sababu ipo nje kalenda ya mechi za shirikisho hilo.
    Nipeni mikoba; Charles Mishetto kushoto akicheza Ujerumani
    Boniface Wambura, Ofisa Habari na Mwasiliano wa  TFF alisema jana mchana kuwa wawili hao hawatakuwamo kwenye kikosi cha kovha mpya Mholanzi Mart Nooij kitakachoivaa Zimbabwe mwishoni mwa wiki ijayo kwa vile wanahitajika kwenye klabu yao.
    Lakini Mishetto anayechezea klabu ya SPBGG 1914 Selbitz ya Ujerumani ameiambia BIN ZUBEIRY jana kutoka nchini humo; “Kama TFF wataweza kuandika barua kwa klabu yangu inaweza kuniruhusu waje wanione, wakiona nitawafaa, sawa wakiona siwezi nitarudi, ila naamini ninaweza kuisaidia timu yangu,”.
    Charles Mishetto ameendelea kung’ara katika Ligi Daraja la Nne Ujerumani baada ya mwishoni mwa wiki kufunga bao moja timu yake ikilala 2-1 mbele ya SVO 1912 ugenini.
    Katika mchezo huo Ligi Daraja la Nne, iitwayo Bayernliga 4, Michael Johnson aliwafungia wenyeji dakika ya 10 na Ricko Muller akafunga la pili dakika ya 26, kabla ya Mishetto kuifungia Selbitz dakika ya 62.
    Mishetto aliangushwa kwenye eneo la hatari siku hiyo na timu yake ikapewa penalti, lakini bahati mbaya yeye mwenyewe akakosa.
    Mechi za kuwania kufuzu AFCON zitafanyika Mei 16-18, tarehe ambayo haipo kwenye ratiba ya FIFA na kwa hivyo haitakuwa lazima wachezaji wa klabu kuruhusiwa kuondoka.
    Hata hivyo, michuano ya makundi itakayoshirikisha Ghana, Nigeria na Cameroon, zitakuwa katika tarehe iliyoidhinishwa na FIFA , ikimaanisha kuwa klabu vya soka kote duniani lazima ziwaruhusu wachezaji wao kushiriki mechi hizo.
    Mbali na Samata na Ulimwengu, wachezaji kama Edward Sadomba, wataathiriwa na mgongano wa tarehe zilizo kati ya mechi za kufuzu zitakazofanyika 2015 na michuano ya klabu. Sadomba atahitajika kwa wakati mmoja na klabu yake ya Al Ahli Benghazi pamoja na timu yake ya taifa Zimbabwe itakayokipiga dhidi ya Taifa Stars.

    Lakini FIFA lilikaririwa na BBC juzi likieleza kuwa wachezaji wanaweza tu kuondoka ikiwa maafisa wa klabu na mashirikisho ya nchi husika wanaweza kukubaliana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTANZANIA ANAYECHEZA UJERUMANI AOMBA KUZIPA PENGO LA SAMATTA TAIFA STARS Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top