// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); KINDA LAIPA USHINDI MAN UNITED KOCHA GIGGS AKIICHEZA NGOMA MWENYEWE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE KINDA LAIPA USHINDI MAN UNITED KOCHA GIGGS AKIICHEZA NGOMA MWENYEWE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, May 06, 2014

    KINDA LAIPA USHINDI MAN UNITED KOCHA GIGGS AKIICHEZA NGOMA MWENYEWE

    KINDA wa umri wa miaka 18, James Anthony Wilson usiku huu ameifungia Manchester United mabao mawili ikishinda 3-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England, Uwanja wa Old Trafford mjini Manchester dhidi ya Hull City.
    Bwana mdogo huyo alifunga bao la kwanza dakika ya 31 na la pili dakika ya 61, wakati bao la Hull City lilifungwa na Matt Fryatt dakika ya 63 kabla ya Robin van Persie kuwafungia Mashetani Wekundu la tatu dakika ya 86.
    Watoto tunaweza; Kinda James Wilson akishangilia baada ya kufunga usiku huu
    Ushindi huo, unaifanya United itimize pointi 63 baada ya kucheza mechi 36, ikiendelea kubaki nafasi ya saba nyuma ya Tottenham Hotspur yenye pointi 66 za mechi 37.
    Kocha wa muda wa United, Ryan Giggs leo kwa mara ya kwanza alicheza tangu aanze kukaimu nafasi ya David Moyes wiki mbili zilizopita, akiingia kuchukua nafasi ya Thomas Lawrence dakika ya 70 sawa na Nemanja Vidic aliyempokea Phil Jones dakika ya 22 na Van Persie aliyemrithi Wilson dakika ya 64.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KINDA LAIPA USHINDI MAN UNITED KOCHA GIGGS AKIICHEZA NGOMA MWENYEWE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top