• HABARI MPYA

    Saturday, October 31, 2009

    BUSTA RHYMES ANAYEKUJA KUWASHIKA FIESTA 2009 ONE LUV




    NILIPOISIKIA kwa mara ya kwanza sauti yake kwenye matangazo ya kituo cha Radio Clouds, akiwaambia Watanzania kwamba atakuwapo kutumbuiza kwenye Fiesta ya 2009, awali nilidhani ni Ja Rure anakuja tena nchini kutumbuiza kwenye tamasha ambalo aliwahi kutumbuiza mwaka 2006.
    Lakini nilipotulia na kusikiliza hadi mwisho wa tangazo hilo— jina lililotajwa lilikwenda sambamba na dhana niliyokuwa nayo ama atakuwa Ja Rule au Busta Rhymes. Kweli, Busta Rhymes anakuja Tanzania kufanya onyesho moja, akiletwa na kampuni ya Prime Time Promotion Limited, chini ya udhamini wa Serengeti Beer na Nokia.
    Ama kweli Fiesta ya mwaka huu itakuwa tamu kuliko zote zilizowahi kufanyika, kwani unapomzungumzia Busta unamaanisha mwanamuziki wa Hip hop anayekubalika na watu wa rika na jinsia zote, yaani wake kwa waume, vijana na hata watu wazima.
    Hiyo inatokana na muziki wake, jinsi anavyoweza kubadilika kulingana na wakati, jambo ambalo limemfanya aendelee kuwa juu siku zote.
    Msikie katika wimbo I Know What You Want aliomshirikisha Mariah Carey: “Baby if you give it to me, I'll give it to you, I know what you want, You know I got it….Baby if you give it to me, I'll give it to you, I know what you want…You know I got it…”.
    Busta ni mkali na kwa sababu hiyo ana haki ya kuwa kipenzi cha wapenzi wa muziki ulimwenguni kote.
    Kwa wakati huu anakuja Tanzania ni muda mfupi tu tangu atoe wimbo wake mpya uitwao Arab Money Remix, ambao ndani yake amewashirikisha wakali wengine P Diddy, Ron Browz, Swizz Beats, T. Pain, Akon na Lil Wayne. Wimbo huu, jamaa wanataja maneno ambayo mengine yapo kwenye Qur’an tukufu kwa mfano kwenye kiitikio cha pili; wanasema;
    Bismillahi r-rahmani r-rahim, Al hamdu lillaahi rabill'alamin (Oooohh),
    We gettin' arab money (haha), We gettin' arab money…Bismillahi r-rahmani r-rahim, Al hamdu lillaahi rabiil'alamin (Oooohh) We gettin' arab money (haha), We gettin' arab money.
    Hili linaweza likasababisha Busta akawa gumzo zaidi katika ujio wake Tanzania, lakini ukweli ni kwamba jamaa ni mkali tangu na tangu.
    Jina Busta Rhymes alitungwa na Chuck D wa kundi la Public Enemy, kutokana na kumfananisha na mchezaji wa zamani wa Ligi ya Taifa mpira Marekani (NFL), George ‘Buster’ Rhymes, lakini mwenyewe jina lake halisi Trevor Tahiem Smith, Jr.
    Huyo ni mwanamuziki, mtunzi wa nyimbo na mwigizaji maarufu duniani, Mmarekani mwenye asili ya Jamaica, aliyezaliwa Mei 20, mwaka 1972 ambaye Novemba 7, mwaka huu atafanya vitu vyake mjini Dar es Salaam, Tanzania.
    Busta alizaliwa East Flatbush, huko Brooklyn, wazazi wake wanatokea Jamaica, Cherry Green na Trevor Smith.
    Busta alianza muziki akiwa ana umri wa miaka 17 baada ya kujiunga na kundi la Hip hop, lililokuwa likijulikana kama Leaders of the New School akiwa sambamba na jamaa zake wa Long Island, Charlie Brown, Dinco D na Cut Monitor Milo. Walianza kurekodi muziki mwaka 1989 na kufanikiwa kutoa albamu yao ya kwanza A Future Without a Past mwaka 1991 kutoka studio za Elektra Records.
    Mwaka 1993, walitopa kitu kingine, kilichokwenda kwa jina T.I.M.E. (The Inner Mind's Eye), lakini kundi hilo lilisambaratika kutokana na wenzake kumwonea wivu Busta kwa sababu ya umaarufu mkubwa aliokuwa amejipatia.
    Hivyo mwaka 1996 alitoa wimbo wake wa kwanza kama msanii binafsi uliokwenda kwa jina la Woo Hah!! Got You All in Check am,bao ulikuwamo kwenye albamu yake iliyouza nakala zaidi ya Milioni, The Coming.
    Albamu yake ya pili When Disaster Strikes, aliitoa mwaka 1997, ambayo ndani yake ilikuwa ni nyimbo kali kama Put Your Hands Where My Eyes Could See na Dangerous.
    Mwaka 1998, Busta alitoa kingine; Extinction Level Event (Final World Front), ambacho kilizua gumzo kutokana na kutabiri kwamba mwaka 2000 ni mwisho wa dunia.
    Wimbo wake Gimme Some More uliokuwa unafanana wa Bernard Herrmann – ulishika namba tano katika chati za muziki nchini Uingereza Januari mwaka 1999, wakati April mwaka huo, wimbo mwingine What's It Gonna Be?! Aaliomshirikisha Janet Jackson, uliingia kwenye kumi bora ya chati za muziki za Marekani na Uingereza.
    Baada ya Busta kusaini mkataba na J Records, lebo iliyoanzishwa na aliyekuwa bosi wa Arista Records, Clive Davis, alitoa albamu kali, akiendelea kuinukuu Biblia kwenye albamu hiyo aliyoipa jina Genesis. Katika albamu hiyo aliwashirikisha wakali wengine kama Mary J. Blige, P. Diddy, Kelis na wengineo.
    Genesis ilibebwa zaidi na nyimbo kama ule aliomshirikisha Kelis, uitwao What It Is, wimbo wake aliotanguliza kutoka kwenye albamu hiyo, Break Ya Neck Novemba mwaka 2001 na wimbo wa mwisho kuutoa, Pass The Courvoisier Part 2, ambao aliwashirikisha watu kama Pharrell na P. Diddy. Lakini pamoja na umaarufu na kuwa na nyimbo hizo kali, albamu hiyo haikuweza kiuvunja rekodi ya mauzo ya albamu yake iliyotangulia.
    Mwaka 2002, Busta alitoa albamu yake ya sita It Ain't Safe No More, ambayo ilifanya vizuri ile mbaya, ikiongozwa na wimbo mtamu zaidi aliomshirikisha Mariah Carey na kundi la Flipmode Squad, uitwao I Know What You Want.
    Nyimbo nyingine kali kutoka kwenye albamu hiyo zilikuwa Make It Clap, aliomshirikisha Spliff Starr ambao baadaye aliutolea Remix akimshirikisha Sean Paul. Baada ya kutoa albamu hiyo, aliachana na J Records na mwaka 2004 alisaini mkataba na kampuni ya Dr. Dre, Aftermath Entertainment.
    Alipojiunga na Aftermath Busta Rhymes alitoa albamu ya saba, The Big Bang, ambayo ilikuwa albamu yake ya kwanza kuuza nakala zaidi ya milioni maishani mwake. Zaidi ya nakala za CD 209,000 ziliuzwa katika wiki ya kwanza tu tangu kutoka kwa albamu hiyo na kuingia kwenye chati za nyimbo 200 za Billboard. Albamu hiyo pia iliibuka kuwa maarufu zaidi ya albamu zake zote nchini Uingereza, ikishika nafasi ya 19.
    Nyimbo kali zaidi zilizokuwamo kwenye albamu hiyo ni pamoja na Touch It, I Love My Chick, aliowashirikisha Kelis na Will.I.Am, New York Shit na In The Ghetto. Albamu hiyo ilimpa ulaji wa kushiriki ziara za wakali kama Mariah Carey iliyoitwa The Adventures of Mimi Tour. Busta baada ya hapo aliimba na Eminem wimbo Touch It Remix Part 5 sambamba na kufanya wimbo na Linkin Park, ulioitwa We Made it akiwashirisha pia Jae Millz na Ne-Yo.
    Julai 17, 2008, Rhymes aliachana na Aftermath baada ya kutofautiana na Jimmy Lovine na baadaye ikaelezwa atajiunga na Universal Motown, ambayo ilitoa albamu yake ya nane Back on My B.S. Mei 19, mwaka huu sambamba na kushiriki albamu ya kwanza ya Asher Roth, iitwayo Asleep in the Bread Aisle.
    Busta Rhymes alitoa albamu yake ya nane Back on My B.S. Mei 19, mwaka huu akiwa na Universal Motown, ambayo ilishika namba tano katika chati za nyimbo 200 za Billboard, ikiuza nakala 56,000 katika wiki ya kwanza na hadi sasa imekwishauza nakala 122,000. Nyimbo ambazo amekwishatoa kutoka kwenye albamu hiyo ni Arab Money aliowashirikisha Ron Browz, Hustler's Anthem '09, aliomshirikisha T-Pain na Respect My Conglomerate. Wimbo World Go Round, aliomshirikisha mwimbaji Muingereza Estelle, aliutoa nchini Ufaransa Aprili 6, mwaka 2009 kabla ya kuutambulisha na Uingereza Julai 13, mwaka huu.
    Kutokana na mgogoro wa utumiaji maneno kwenye wimbo Arab Money, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) uliifungia albamu hiyo, Back on My B.S. ambayo ilisambazwa kimataifa.
    Kwa mujibu wa Baraza la Habari la Taifa (Marekani), mashairi ya wimbo huo yanawadhalilisha Waarabu na Waislamu, hivyo kunyimwa ruhusa ya kuisambaza albamu hiyo. Baadhi ya ma-DJ, wasanii na mashabiki wameushambulia wimbo huo wakisema unaudhalilisha Uarabu.
    Walisema kwamba sehemu ya wimbo huo katika Remix inanukuu Quran tukufu.
    Hivi karibuni wakati wimbo huo ulipotolewa, DJ Dany Neville na rapa wa Iraqi, The Narcicyst walikasirishwa na wimbo wa Busta Rhymes ambao waliurekodi kama jibu. Baadaye Busta aliomba radhi kwa usumbufu wowote aliousababisha. Ma-DJ nchini humo walisema kwamba, japokuwa hawajapata taarifa yoyote ya kuupiga marufuku wimbo huo kwenye klabu za usiku, lakini hawawezi kuupiga. “Siuchezi wimbo Arab Money kwa sababu umeonyesha dharau kwa Waarabu. Sidhani kama umefungiwa kuchezwa kwenye klabu, lakini wengi hapa hawaupigi kwa vyovyote,” alisema DJ Saif wa Dubai.
    Lakini wakati hayo yakiendelea, Busta alitangaza juu ya ujio wa albamu yake ya tisa itakayojulikana kama The Chemo. Alisema kwa asilimia 80 albamu yake mpya imekwishakamilika, kazi kubwa ikifanywa na mtayarishaji wa Canada, Boi-1da. Yote kwa yote, Busta atakuwapo Dar es Salaam, kuwapa raha Watanzania katika Fiesta ambayo mwaka huu imepewa kaulimbiu ya One Love. Karibu Tanzania Busta.


    WIMBO ULIOLETA BALAA NI HUU HAPA;
    BUSTA:
    Ayo somebody tell steven speilberg & george lucas
    Thank you for directing this movie (hahahaha) (hashemeke hayla ha-its the remix!)

    KIITIKIO x2
    Bismillahi r-rahmani r-rahim, Al hamdu lillaahi rabill'alamin (Oooohh)
    We gettin' arab money (haha), We gettin' arab money
    Bismillahi r-rahmani r-rahim, Al hamdu lillaahi rabiil'alamin (Oooohh)
    We gettin' arab money (haha), We gettin' arab money

    BUSTA
    you can talk about your money but i really dont care
    im into coppin streets shit im trying to buy air
    im the first black nigga that i rap trillionaire
    i control heat i'm bout to buy the ozone layer
    im into coppin minerals now diamonds and granite
    so much paper i could probably gift wrap a planet
    and clone a million janet's respect my company
    asalamalaikumarahmatullahe wa barakatuhu

    KIITIKIO x2

    P DIDDY
    ayo busta we gettin this money for a long time mayne
    check this out
    allahamdulliah with my billions pilin
    im just wildin, bought two islands
    lakshmi makalen
    diamond soundin
    bout to buy japan, trick im just stylin
    money insane
    my generals poppin bottle
    i was buyin out planes just to fly around spain
    fuck a recession im still investin
    bout to buy dubai and swim in the shark section
    get the dark section (its the remix)
    bitch thats the barack section

    KIITIKIO x2 (we gettin bad boy money)

    RON BROWZ
    catch me in da coop that cost a hundred thous,
    hakala shikmina lady ron browz
    my money make noise yours quite as a mouse
    send a email in da boyz in da house
    all da girls love me, ya pop bubbly.
    hakalashikrhi shorty damn ugly
    findin me in the dance floor doin the dougie
    trucks sittin too next to yo buggy

    KIITIKIO
    UBETI WA NNE Swizz Beats
    dont even call me swizz no more
    call me kaseem dean ?
    when i come thru hit you with the brand new
    buggati coupe, damn thing only only sits 2
    but you know who who ridin in my passenger
    side with me flyin shit 2.5 in it, hey hey hey
    im in my jeezy watchin tv she call me her habibi
    while she feedin me linguini
    left right left right and arab dance poppin right
    swizz beats busta, money money buss pipes

    KIITIKIO x2

    T PAIN
    Nappy Boy (halalalla)
    i let my chain hang down with the best of dem
    teddy pain rain down on the rest of dem
    misses troopa man heavy holly
    get em man, about a man, rubber band, droppin money
    bombs like a taliban (hallalla) we gettin arab money (money)
    u want this hook you gon' pay dat money
    save dat money give it to my kids, ill take that hundred
    give her all my kids like (hallalallalalalallaaaaaaaaaa swag)

    KIITIKIO x2 (swaggg swagg)

    AKON
    akon, konvikt, (we gettin arab money swag tpain yelling we gettin arab money)
    musikkkk
    i got dat arab money (money)
    four- star bismillahirahmanirahim
    straight cash wanna keep on comin
    lemme exchange da currency coz its so foreign
    i got dat arab money (money) makin upto 5 kind
    your minds on the money, diamond mine still runnin
    on all of africa you can ask tarzan

    KIITIKIO x1 (heyyyyyyyyyyyyyy)
    senegal! (we gettin arab money)
    senegal! (we gettin arab money)
    yay!
    chorus x1 (heyyyyyyyyyy)
    konvikt (we gettin arab money) (alright boyz)
    konvikttttt musikkk (we gettin arab money)

    LIL WAYNE
    khaled dar say gettin money errday
    his smile look like iced out perrier
    bury me a g and tell ma kids that i was
    now jump into ya grave do you dig what i dug
    cash money universe, my old town check
    20 chains look like a scarf on my neck
    young money entertainment the girls theyre fine
    (and buck a motherfucka money hall of fame) (arab money)
    ya!

    KIITIKIO x2
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    1 comments:

    phpjustme said... March 26, 2010 at 7:24 AM

    He is so handsome!can i love you ?

    Item Reviewed: BUSTA RHYMES ANAYEKUJA KUWASHIKA FIESTA 2009 ONE LUV Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top