• HABARI MPYA

    Friday, January 23, 2026

    NAMUNGO FC YAICHAPA COASTAL UNION 1-0 RUANGWA


    TIMU ya Namungo FC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
    Bao pekee la Namungo FC lililowaduwaza Coastal Union limefungwa na mshambuliaji Mkongo, Fabrice Ngoy wa Ngoy dakika ya 47.
    Kwa ushindi huo, Namungo FC inafikisha pointi 15 katika mchezo wa tisa na kusogea nafasi ya nne, wakati Coastal Union inabaki na pointi zake tisa za mechi 10 sasa nafasi ya 13 kwenye Ligi ya timu 16.
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAMUNGO FC YAICHAPA COASTAL UNION 1-0 RUANGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top