• HABARI MPYA

    Tuesday, January 06, 2026

    NIGERIA YAENDA ROBO FAINALI KIBABE, YAIKANDA MSUMBIJI 4-0


    TIMU ya Nigeria imefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Msumbiji usiku wa jana Uwanja wa Fez mjini  Fez nchini Morocco. 
    Mabao ya Super Eagles yamefungwa na washambuliaji, Ademola Lookman  wa Atalanta ya Italia dakika ya 20, Victor Osimhen wa Galatasaray ya Uturuki mawili, dakika ya 25 na 47 na   Akor Adams wa  Sevilla ya Hispania dakika ya 75.
    Nigeria sasa itakutana na Misri katika Robo Fainali ambayo jana iliitoa Benin kwa kuichapa mabao 3-1 Uwanja wa Adrar mjini Agadir.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NIGERIA YAENDA ROBO FAINALI KIBABE, YAIKANDA MSUMBIJI 4-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top