• HABARI MPYA

    Monday, January 12, 2026

    BARCELONA WAICHAPA REAL 3-2 NA KUTWAA SUPER CUP YA HISPANIA


    TIMU ya Barcelona imefanikiwa kutwaa taji la Super Cup ya Hispania baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Real Madrid usiku wa jana Uwanja wa King Abdullah Sports City Jijini Jeddah, Saudi Arabia.
    Mabao ya Barcelona yamefungwa na  washambuliaji, Mbrazil Raphael Dias Belloli ‘Raphinha’ mawili dakika ya  36 na 73 na Mpoland, Robert Lewandowski  dakika ya 45’+4, wakati ya Real Madrid yamefungwa na washambuliaji pia, Mbrazil Vinícius José Paixão de Oliveira Júnior dakika ya 45’+2 na Mspaniola, Gonzalo García Torres dakika ya 45’+6.
    Barcelona ilifika Fainali ya Super Cup ya Hispania baada ya kuitoa Athletic Bilbao kwa kuichapa 5-0 na Real Madrid ikishinda 2-1 dhidi ya ya Atlético Madrid mechi zote zikipigwa Uwanja wa King Abdullah Sports City Jijini Jeddah.
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARCELONA WAICHAPA REAL 3-2 NA KUTWAA SUPER CUP YA HISPANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top