MABAO ya viungo Zidane Ally Sereri dakika ya tano na Himid Mao Mkami dakika ya 54 yameipa Azam FC ushindi wa 2-0 dhidi ya waliokuwa mabingwa watetezi, Mlandege FC katika mchezo wa Kundi A Kombe la Mapinduzi usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Azam FC inafikisha pointi nne baada ya ushindi huo kufuatia sare ya kufungana bao 1-1 na Singida Black Stars katika mchezo wa kwanza hapo hapo Amaan Complex.
Mlandege inakamilisha mechi zake tatu za Kundi A kwa kufungwa zote, nyingine 3-1 na Singida Black Stars na 1-0 na URA FC ya Uganda.
Sasa timu za Azam FC na Singida Black Stars zitahitaji kushinda dhidi ya URA ili kupata tiketi ya kwenda Nusu Fainali.
Mlandege inakamilisha mechi zake tatu za Kundi A kwa kufungwa zote, nyingine 3-1 na Singida Black Stars na 1-0 na URA FC ya Uganda.
Sasa timu za Azam FC na Singida Black Stars zitahitaji kushinda dhidi ya URA ili kupata tiketi ya kwenda Nusu Fainali.



.png)
0 comments:
Post a Comment