TIMU ya Azam FC imefanikiwa kwenda Hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 1-0 dhidi ya Mbeya Kwanza usiku huu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini dar es Salaam.
Bao pekee la Azam FC, moja ya timu tishio za Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara lililoitupa nje Mbeya Kwanza inayoshiriki Ligi ya Championship limefungwa na winga Iddi Suleiman Ally 'Nado' dakika ya 11 akimalizia kazi nzuri ya beki wa kulia, Nathaniel Raphael Chilambo.
Nayo Singida Black Stars imefanikiwa kwenda Hatua ya 16 Bora Kombe la CRDB kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Songea United leo Uwanja wa Mwigulu Airtel Complex mkoani Singida.
Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na mshambuliaji Mkenya, Elvis Rupia, kiungo Mghana, Emmanuel Kwame Keyekeh kwa penalti na mshambuliaji mwingine, Muivory Coast, Joseph Gnadou Guede.
Bao pekee la Azam FC, moja ya timu tishio za Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara lililoitupa nje Mbeya Kwanza inayoshiriki Ligi ya Championship limefungwa na winga Iddi Suleiman Ally 'Nado' dakika ya 11 akimalizia kazi nzuri ya beki wa kulia, Nathaniel Raphael Chilambo.
Nayo Singida Black Stars imefanikiwa kwenda Hatua ya 16 Bora Kombe la CRDB kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Songea United leo Uwanja wa Mwigulu Airtel Complex mkoani Singida.
Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na mshambuliaji Mkenya, Elvis Rupia, kiungo Mghana, Emmanuel Kwame Keyekeh kwa penalti na mshambuliaji mwingine, Muivory Coast, Joseph Gnadou Guede.
Nayo Mbeya City imeitoa Bandari FC kwa kuichapa 3-0 mabao ya Vitalis Mayanga dakika ya 16 na 55 na Riphat Msuya dakika ya 76 Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Ilikuwa siku mbaya kwa timu mbili za Ligi Kuu, Tanzania Prisons na Mtibwa Sugar ambazo zimetolewa na timu za Championship kwa vipigo vinavyofanana nyumbani, 1-0 zote.
Mtibwa Sugar imefungwa 1-0 na Mbuni FC ya Arusha bao la Omary Athumani dakika ya 33 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, wakati Tanzania Prisons imefungwa 1-0 na TMA Stars ya Arusha pia bao la Ernest Baltazari dakika ya 39 Uwanja wa Halmashauri ya Wilaya Chunya Jijini Mbeya.
MATOKEO YOTE 32 BORA KOMBE LA CRDB
Azam FC 1-0 Mbeya Kwanza
Yanga SC 7-1 Polisi Tanzania
Singida Black Stars 3-1 Songea United
Mbeya City 3-0 Bandari FC
Mtibwa Sugar 0-1 Mbuni FC
Tanzania Prisons 0-1 TMA Stars
Fountain Gate 2-1 Gunners FC
Coastal Union 4-1 Stand United
Simba Sc 2-0 B19 FC
Namungo FC 4-1 Kagera Sugar
Pamba Jiji FC 2-1 Transit Camp
Geita Gold 4-1 Nyika FC
Mashujaa FC 0-0 KegGold (Penalti 5-3)
JKT Tanzania 2-0 Hausang FC
TRA United 4-0 Kijiwe Nongwa
Dodoma Jiji 2-0 African Sports




.png)
0 comments:
Post a Comment