• HABARI MPYA

    Wednesday, January 14, 2026

    MANE AIPELEKA SENEGAL FAINALI AFCON


    TIMU ya Senegal imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Misri usiku huu Uwanja wa Tangier Grand Jijini Tangier nchini Morocco.
    Bao pekee la Simba wa Teranga katika mchezo huo mtamu wa Nusu-Fainali AFCON 2025 limefumgwa na mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Sadio Mané ambaye kwa sasa anachezea Al-Nassr ya Saudi Arabia dakika ya 78.
    Senegal sasa itakutana na mshindi wa Nusu Fainali ya pili kati ya wenyeji, Morocco na Nigeria watakaomenyana kuanzia Saa 5:00 usiku Uwanja wa Prince Moulay Abdellah Jijini Rabat.
    Nyota wa Liverpool, Mohamed Salah na wa Manchester City, Omar Marmoush hawakuweza kuwasaidia Mafarao kufurukuta mbele ya Simba wa Teranga. 
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANE AIPELEKA SENEGAL FAINALI AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top