// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); NIGERIA YATAJA KIKOSI CHA KUBEBA KOMBE LA DUNIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE NIGERIA YATAJA KIKOSI CHA KUBEBA KOMBE LA DUNIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, May 07, 2014

    NIGERIA YATAJA KIKOSI CHA KUBEBA KOMBE LA DUNIA

    SHIRIKISHO la Soka Nigeria (NFF) limetangaza kikosi cha cha awali cha wachezaji 30 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia la FIFA nchini Brazil baadaye mwaka huu.
    Kutangazwa kwa wachezaji hao jana, kumefutia kikao cha pamoja baina ya NFF na kocha wa Super Eagles, Stephen Keshi.
    Kikosi hicho ni makipa; Vincent Enyeama, Austin Ejide, Chigozie Agbim na Daniel Akpeyi; Mabeki: Elderson Echiejile, Juwon Oshaniwa, Godfrey Oboabona, Azubuike Egwuekwe, Kenneth Omeruo, Joseph Yobo, Kunle Odunlami na Efe Ambrose.
    Kocha wa Nigeria, Stephen Kheshi ametaja kikosi cha wachezaji 30 cha awali kwa ajili ya Kombe la Dunia
    Viungo: John Mikel Obi, Ogenyi Onazi, Ramon Azeez, Joel Obi, Nosa Igiebor, Michael Uchebo, Ejike Uzoenyi, Sunday Mba na Reuben Gabriel, wakati washambuliaji ni: Ahmed Musa, Shola Ameobi, Emmanuel Emenike, Obinna Nsofor, Osaze Odemwingie, Babatunde Michael, Victor Moses, Uche Nwofor na Nnamdi Oduamadi.
    Nigeria ni moja kati ya nchi tano za Afrika zitakazoshiriki fainali za Kombe la dunia mwaka huu, pamoja na Algeria, Ghana na Ivory Coast.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NIGERIA YATAJA KIKOSI CHA KUBEBA KOMBE LA DUNIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top