KIPA wa Arsenal na Jamhuri ya Czech Republic, Petr Cech ametangaza kustaafu ya soka ya kimataifa.
Mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 34 anashikilia rekodi ya kuichezea mechi 121 nchi yake na alicheza mechi zote tatu kikosi cha Pavel Vbra kikitolewa hatua ya makundi Euro 2016 Ufaransa kwa kuambulia pointi moja tu.
Cech alianza kucheza soka ya kimataifa mwaka 2002 na akaichezea Jamhuri ya Czech katika Euro ya 2004 - ambako walishika nafasi ya tatu - na Kombe la Dunia 2006 kabla ya kurudi kwenye Euro 2008.
0 comments:
Post a Comment