WENYEJI, JKT Tanzania wameiadhibu Pamba Jiji FC kwa kuitandika mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara ISIJI hui Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam.
Mabao ya JKT Tanzania yamefungwa na mshambuliaji Valentino Mashaka Kusengama mawili dakika ya 34 na 70 na winga Saleh Karabaka Kikuya dakika ya 55.
Kwa ushindi huo, JKT Tanzania inafikisha pointi 24 katika mchezo wa 14 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu, wakati Pamba Jiji FC inabaki na pointi zake 17 za mechi 12 nafasi ya tano.


.png)
0 comments:
Post a Comment