WENYEJI, Coastal Union wamelazimishwa sars ya kufungana bao 1-1 na TRA United ya Tabora katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Mkongwe Shiza Ramadhani Kichuya alianza kuifungia Coastal Union kwa penalti dakika ya 35, kabla ya winga Denis Nkane anayecheza kwa mkopo kutoka Yanga kuisawazishia TRA United dakika ya 48.
Kwa matokeo hayo, Coastal Union inafikisha pointi 11 katika mchezo wa 12 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 11 kwenye ligi ua timu. 16, wakati TRA United inafikisha pointi 13 katika mchezo wa 10 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya nane.



.png)
0 comments:
Post a Comment