• HABARI MPYA

    Sunday, July 17, 2016

    WILDER AMMALIZA ARREOLA RAUNDI YA NANE NA KUTETEA TAJI

    Bondia Deontay Wilder (kushoto) akimchapa konde Mmarekani mwenzake, Chris Arreola katika pambano lao la uzito wa juu usiku wa kuamkia leo ukumbi wa Legacy Arena mjini Alabama, Marekani. Wilder alishinda kwa Technical Knockout (TKO) raundi ya nane baada ya mpinzani wake kujiuzulu na kutetea taji lake la WBC uzito wa juu. Hata hivyo, Wilder alivunjika mkono katika pambano hilo, hivyo uwezekano wa kurudi ulingoni haraka kwa ajili ya pambano ama na Anthony Joshua au Tyson Fury ni mdogo sasa PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WILDER AMMALIZA ARREOLA RAUNDI YA NANE NA KUTETEA TAJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top