TIMU za Wydad Casablanca ya Morocco na Mamelodi Sundowns zinaongoza maakundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya mechi za katikati ya wiki hii.
Wydad Casablanca iliifunga 2-0 Zesco United juzi mjini Casablanca na kufikisha pointi sita katika Kundi A, mbele ya ASEC Mimosa iliyoshinda 2-1 ugenini dhidi ya Al Ahly mjini Cairo Misri na kupata pointi tatu za kwanza, wakati Zesco pia ina pointi tatu na Al Ahly haina pointi inashika mkia.
Mamelodi Sundowns ilishinda 2-1 nyumbani dhidi ya Enyimba ya Nigeria Jumanne na kupata pointi tatu za kwanza hivyo kuongoza Kundi B kwa wastani wa mabao, ikilingana pointi na Zamalek ya Misri ambayo haikuwa na mechi baada ya CAF kuiondoa ES Setif ya Algeria mashindanoni kwa vurugu za mashabiki wake.
Enyimba inashika mkia katika kundi hilo ikiwa haina pointi baada ya kucheza mechi, tofauti na wapinzani wake, Mamelodi na Zamalek ambazo kila moja imecheza mechi moja.
ES Setif iliondolewa kufuatia vurugu kubwa zilizofanywa na mashabiki wake katika mchezo dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini Juni 19 iliyopita.
Ripoti ya marefa ilisema amani ilichafuka uwanjani baada ya mashabiki kurusha mioto, chupa na mawe na kusababisha watu kadhaa kujeruhiwa kabla ya walinzi kuingilia kati kutuliza hali hiyo.
Wydad Casablanca iliifunga 2-0 Zesco United juzi mjini Casablanca na kufikisha pointi sita katika Kundi A, mbele ya ASEC Mimosa iliyoshinda 2-1 ugenini dhidi ya Al Ahly mjini Cairo Misri na kupata pointi tatu za kwanza, wakati Zesco pia ina pointi tatu na Al Ahly haina pointi inashika mkia.
Mamelodi Sundowns ilishinda 2-1 nyumbani dhidi ya Enyimba ya Nigeria Jumanne na kupata pointi tatu za kwanza hivyo kuongoza Kundi B kwa wastani wa mabao, ikilingana pointi na Zamalek ya Misri ambayo haikuwa na mechi baada ya CAF kuiondoa ES Setif ya Algeria mashindanoni kwa vurugu za mashabiki wake.
Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini inaongoza Kundi B Ligi ya Mabingwa Afrika |
ES Setif iliondolewa kufuatia vurugu kubwa zilizofanywa na mashabiki wake katika mchezo dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini Juni 19 iliyopita.
Ripoti ya marefa ilisema amani ilichafuka uwanjani baada ya mashabiki kurusha mioto, chupa na mawe na kusababisha watu kadhaa kujeruhiwa kabla ya walinzi kuingilia kati kutuliza hali hiyo.
Kundi A
Na | Timu | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Wydad Casablanca | 2 | 2 | 0 | 0 | 3 | 0 | 3 | 6 |
2 | ASEC Mimosas | 2 | 1 | 0 | 1 | 2 | 2 | 0 | 3 |
3 | Zesco United | 2 | 1 | 0 | 1 | 3 | 4 | -1 | 3 |
4 | Al Ahly | 2 | 0 | 0 | 2 | 3 | 5 | -2 | 0 |
Kundi B
Na | Timu | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Mamelodi Sundowns | 1 | 1 | 0 | 0 | 2 | 1 | 1 | 3 |
2 | Zamalek | 1 | 1 | 0 | 0 | 1 | 0 | 1 | 3 |
3 | Enyimba | 2 | 0 | 0 | 2 | 1 | 3 | -2 | 0 |
0 comments:
Post a Comment