N'Golo Kante (katikati) akiwa na tuzo yake ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa Chelsea PICHA ZAIDI GONGA HAPA
KIUNGO wa kimataifa wa Ufaransa, N'Golo Kante ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa msimu wa Chelsea kwa mara ya pili mfululizo.
Kiungo ameendelea kung'ara Chelsea ingawa haikuwa katika msimu mzuri akitwaa tuzo hiyo kwa mara ya pili mfululizo.
Mchezaji mwenzake, Mbrazil Willian amefanikiwa kuchukua tuzo mbili usiku wa jana West Kensington, akishinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Wachezaji na Bao Bora la Msimu.
Usiku wa jana pia ilishuhudiwa wachezaji na viongozi wakijumuika pamoja kushangilia mafanikio ya msimiu.
Tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka imechukuliwa na Andreas Christensen, Mchezaji Bora wa Mwaka wa Chelsea ya Wanawake ni Fran Kirby na Mchezaji Bora wa Msimu wa Akademi ni Reece James.
Tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka imechukuliwa na Andreas Christensen, Mchezaji Bora wa Mwaka wa Chelsea ya Wanawake ni Fran Kirby na Mchezaji Bora wa Msimu wa Akademi ni Reece James.
0 comments:
Post a Comment