• HABARI MPYA

    Wednesday, May 23, 2018

    RASMI, UNAI EMERY NDIYE KOCHA MPYA WA ARSENAL

    Unai Emery ametambulishwa rasmi kuwa kocha mpya wa Arsenal akichukua nafasi ya Arsene Wenger PICHA ZAIDI GONGA HAPA  


    WASIFU WA KOCHA UNAI EMERY  

    Kuzaliwa: Hondarribia, Hispania Novemba 3, 1971

    MCHEZAJI

    Alianzia Real Sociedad, akacheza mechi tano za La Liga wingi ya kushoto kabla ya kuhamia Toledo ya Daraja la Pili.

    KOCHA

    2005-06 Lorca Deportiva Akaipandisha Daraja la Pili kwa mara ya kwanza 
    2006-08 Almeria
    Akaipandisha Ligi Kuu kwa mara ya kwanza kwenye historia ya klabu
    2008-12 Valencia
    Wakashika nafasi ya tatu mfululizo katika La Liga 
    2012 Spartak Moscow
    Akapoteza mechi 11 katika miezi sita. Akafukuzwa baada ya kufungwa 5-1 nyumbani na Dynamo Moscow. 
    2013-16 Sevilla
    Akashinda mataji matatu mfululizo ya Europa League 
    2016-18 Paris Saint-Germain
    Akashinda mataji yote matatu ya nyumbani 
    Matokeo ya Ukocha
    Amecheza mechi 719, ameshinda 385, sare 155, amefungwa 179 na asilimia ya ushindi 53.5 
    MATAJI
    Sevilla
    Europa League (x3): 2014, 2015, 2016
    Paris Saint-Germain
    Ligue 1: 2017-18
    Kombe la Ufaransa (x2): 2017, 2018
    Kombe la Ligi Ufaransa (x2): 2017, 2018
    Super Cup ya Ufaransa (x2): 2016, 2017


    KOCHA Unai Emery amesema kwamba amepewa heshima ya kujiunga na klabu kubwa baada ya kutangazwa kuchukua nafasi ya Arsene Wenger klabu ya Arsenal kwa mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya Pauni Milioni 15.
    Kocha huyo wa zamani wa Paris Saint-Germain amempiku kiungo wa zamani wa Arsenal, Mikel Arteta katika kuwania nafasi hiyo ya kazi Uwanja wa Emirates.
    Emery sasa anakwenda kuchukua mikoba iliyoachwa na Wenger, ambaye amekuwa kazini Kaskazini mwa London kwa zaidi ya miaka 22.
    Arsenal imefichua habari hizo Saa 3 asubuhi ya leo kwa mumtangaza Emery: "Mpya ametua. Zama mpya. Ukurasa mpya,". Mspaniola huyo atatangazwa rasmi katika mkutano na Waandishi wa Habari mchana wa leo.
    Historia ya Emery inaanzia alipokuwa mchezaji wa Real Sociedad ambako alicheza mechi tano za La Liga wingi ya kushoto kabla ya kuhamia Toledo ya Daraja la Pili.
    Mwaka 2005-2006 akageukia ukocha akianza na klabu ya Lorca Deportiva aliyoipandisha Daraja la Pili kwa mara ya kwanza, kabla ya mwaka 2006-08 kwenda Almeria ambayo aliipandisha Ligi Kuu kwa mara ya kwanza kwenye historia ya klabu hiyo.
    Mwaka 2008 akaenda Valencia ambako alidumu hadi 2012 akiiwezesha kushika nafasi ya tatu mara tatu mfululizo katika La Liga, kabla ya kuhamia Spartak Moscow, ambako hata hivyo hakudumu, kwani baada ya kupoteza mechi 11 katika miezi sita alifukuzwa baada ya kufungwa 5-1 nyumbani na Dynamo Moscow. 
    Akaenda Sevilla ambako alishinda mataji matatu mfululizo ya Europa League kati ya 2013 na 2016 kabla ya kujiunga na PSG mwaka 2016 ambako alishinda mataji yote matatu ya nyumbani na sasa anaingia Arsenal. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RASMI, UNAI EMERY NDIYE KOCHA MPYA WA ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top