• HABARI MPYA

    Tuesday, July 24, 2012

    SIMBA WAMDHALILISHA MAMA MMOJA TAIFA HADI HURUMA









    Mashabiki wa Simba, leo wamemtembezea kichapo mama mmoja aliyekuwa amevalia jezi ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars yenye nembo ya Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), kosa kukaa kwenye jukwaa walilokuwa wamekaa wao. Sasa haikuweza kufahamika mara moja, mashabiki wa Simba wana bifu na TFF au hawapendi timu ya taifa. Mama huyo alikimbizwa huku akipewa kichapo hadi kutokwa damu, kabla ya kuokolewa na Polisi waliomteremsha jukwaani. Aliporwa vitu vyake kama pochi na kadhalika. Baadaye akiwa amekwishaokolewa na askari, ndipo msamaria mwema mmoja, albino akamuokotea baadhi ya vitu na kuwakabidhi askari. Huwezi kulipa jina lingine tukio lile, zaidi ya udhalilishaji wa kijinsia. Alikuwa anatia huruma mama huyo wakati anahangaika kujitoa kwenye kundi la mashabiki wa kiuma wa Simba, iliyofungwa 3-1 na Azam leo katika Robo Fainali ya Kombe la Kagame.      
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA WAMDHALILISHA MAMA MMOJA TAIFA HADI HURUMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top