• HABARI MPYA

    Wednesday, July 25, 2012

    ISSA KIHANGE AFARIKI DUNIA UWANJANI AKICHEZA


    KIUNGO wa zamani wa Simba SC, Issa Kihange amefariki dunia jana maeneo ya nyumbani kwake, Mbezi Jogoo, baada ya kuanguka uwanjani wakati akicheza mechi za maveterani.
    Kwa mujibu wa kiungo wa zamani wa Yanga, Waziri Mahadhi ‘Mandieta’ aliyekuwapo maeneo ya tukio, alisema kwamba baada ya Kihange kuanguka wakati akishangilia bao alilofunga mazoezini uwanjani, alikimbizwa hospitali ya IMTU, ambako umauti ulimfika.
    Issa Kihange alikuwamo na aling’ara kwenye kikosi cha Simba kilichotwaa taji la pili Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mwaka 1991 mjini Dar es Salaam.  BIN ZUBEIRY kwa sasa anafuatilia taarifa zaidi, ili kujua mchezaji huyo atazikwa lini na wapi.   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ISSA KIHANGE AFARIKI DUNIA UWANJANI AKICHEZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top