• HABARI MPYA

    Saturday, January 16, 2016

    KIIZA ‘DIEGO’ AING’ARISHA SIMBA SC, YAILAZA MTIBWA 1-0 TAIFA, SASA YAIPUMULIA YANGA

    RATIBA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA;
    Januari 16, 2016
    Simba SC 1-0 Mtibwa Sugar
    JKT Ruvu 1-5 Mgambo JKT
    Toto Africans 0-1 Prisons
    Stand United 1-0 Kagera Sugar
    Mbeya City 1-0 Mwadui FC
    Coastal Union 1-1 Majimaji
    Azam FC Vs African Sports (Saa 1:00 usiku)
    Januari 17, 2016
    Yanga SC Vs Ndanda FC

    Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
    BAO pekee la mshambuliaji Hamisi Friday Kiiza ‘Diego’ limeipa Simba SC ushindi wa 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uganda, Kiiza aliifungia Simba SC bao hilo dakika ya tano tu kwa kichwa akimalizia krosi nzuri ya Ibrahim Hajib kutoka upande wa kushoto.
    Na sasa Simba SC inafikisha pointi 30 baada ya kucheza mechi 14, ikiendelea kukaa nafasi ya tatu nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga SC pointi 32 za mechi 13 na vinara, Azam FC pointi 35 za mechi 13 pia.
    Azam FC watacheza mechi yao ya 14 usiku wa leo dhidi ya African Sports ya Tanga Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, wakati Yanga SC watakuwa wenyeji wa Ndanda Uwanja wa Taifa kesho.
    Wachezaji wa Simba SC wakimpongeza Hamisi Kiiza (kushoto) baada ya kufunga leo Uwanja wa Taifa

    Pamoja na kufungwa, Mtibwa Sugar walionyesha upinzani kwa Simba SC na dakika ya 11, kiungo Shiza Kichuya alipoteza nafasi ya wazi baada ya shuti lake kuokolewa na kipa Vincent Angban, raia wa Ivory Coast.
    Dakika ya 44, Ally Shomari naye alipiga shuti kali, lakini kipa wa Simba SC, Vincent Angban akaokoa.
    Kizza naye alipoteza nafasi za kufunga dakika ya 15 na 33 baada ya kupiga nje.
    Kipindi cha pili, timu zote ziliendelea kushambuliana kwa zamani, lakini matokeo hayakubadilika. 
    Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Vincent Angban, Emery Nimubona, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Hassan Isihaka, Juuko Murshid, Justice Majabvi, Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude, Ibrahim Hajib/Danny Lyanga dk64, Hamisi Kiiza/Awadh Juma dk89 na Peter Mwalyanzi/Said Ndemla dk31.
    Mtibwa Sugar; Said Mohamed, Ally Shomary, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Salim Mbonde, Henry Joseph, Shaaban Nditi, Shiza Kichuya, Muzamil Yassin, Hussein Javu/Jaffar Kibaya dk64, Ibrahim Rajab ‘Jeba’ na Mohammed Ibrahim/Vincent Barnabas dk64.
    Mechi nyingine za Ligi Kuu leo; Prisons imeifunga Toto 1-0 Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Stand United imeifunga 1-0 Kagera Sugar Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Mbeya City imeifunga 1-0 Mwadui FC Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Coastal Union imelazimishwa sare ya 1-1 na Majimaji Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
    Mchezo kati ya vinara wa Ligi Kuu, Azam FC dhidi ya African Sports unafuatia sasa Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, wakati kesho mabingwa watetezi, Yanga wataikaribisha Ndanda FC ya Mtwara.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIIZA ‘DIEGO’ AING’ARISHA SIMBA SC, YAILAZA MTIBWA 1-0 TAIFA, SASA YAIPUMULIA YANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top