• HABARI MPYA

    Sunday, January 31, 2016

    MGAMBO JKT YALAZIMISHWA SARE 1-1 NA NDANDA FC MKWAKWANI

    MATOKEO LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
    Januari 30, 2016
    Coastal Union 2-0 Yanga SC
    Simba SC 4-0 African Sports
    JKT Ruvu 0-0 Majimaji
    Mtibwa Sugar 1-0 Stand United
    Mwadui FC 1-0 Toto Africans
    Januari 31, 2016
    Mgambo JKT 1-1 Ndanda FC
    Kagera Sugar 2-0 Mbeya City
    Mgambo JKT wamelazimishwa sare ya 1-1 na Ndanda FC leo Uwanja wa Mkwakwani

    Na Salma Isihaka, TANGA
    MGAMBO Shooting imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Ndanda FC ya Mtwara katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
    Matokeo hayo, yanaifanya Mgambo JKT ifikishe pointi 17 baada ya kucheza mechi 16 na kuendelea kukaa nafasi ya tisa, wakati Ndanda FC inafikisha pointi 13 baada ya kucheza mechi 16, pia wakiendelea kukaa nafasi ya 14 katika Ligi ya timu 16 ambayo mwisho wa msimu mbili zitashuka.
    Chande Magoja alianza kuifungia Mgambo JKT dakika ya 51, kabla ya Omar Mponda kuisawazishia Ndanda FC dakika ya 77.
    Mechi nyingine za Ligi Kuu jana, Coastal Union waliifunga 2-0 Yanga SC Mkwakwani, Simba SC iliitandika 4-0 African Sports Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, JKT Ruvu ilitoka sare ya 0-0 na Majimaji Uwanja wa Karume, Mtibwa Sugar ikashinda 1-0 dhidi ya Stand United na Mwadui FC ikashinda 1-0 dhidi ya Toto Africans.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MGAMBO JKT YALAZIMISHWA SARE 1-1 NA NDANDA FC MKWAKWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top