• HABARI MPYA

    Thursday, January 21, 2016

    LIVERPOOL YASHINDA 3-0 NA KUFUZU RAUNDI YA NNE KOMBE LA FA ENGLAND

    Mshambuliaji wa Liverpool, Christian Benteke akipiga kichwa kilichoenda juu ya lango la Exeter City katika mchezo wa marudiano wa Raundi ya Tatu Kombe la FA England. Liverpool ilishina 3-0 usiku wa jana Uwanja wa Anfield, mabao ya Joe Allen, Sheyi Ojo na Joao Teixeira na kufuzu Raundi ya Nne, ambako itakutana na West Ham United PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    Mshambuliaji wa kimataifa wa Korea Kusini, Son Heung-min (kushoto) akifumua shuti kuifungia Tottenham Hotspur bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Leicester City kwenye mchezo wa marudiano Raundi ya Tatu Kombe la FA England Uwanja wa King Power. Bao lingine la Spurs limefungwa na Nacer Chadli na sasa itamenyana na Colchester United ugenini katika Raundi ya Nne PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YASHINDA 3-0 NA KUFUZU RAUNDI YA NNE KOMBE LA FA ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top