• HABARI MPYA

    Saturday, January 23, 2016

    MAN UNITED YAKARIBIA KUINASA SAINI YA 'MIDO HATARI' LA BENFICA

    KLABU ya Manchester United imekaribia kumsajili kiungo Renato Sanches baada ya mazungumzo kwenda vizuri jana mjini London.
    KInda huyo wa umri wa miaka 18 wa Benfica thamani yake ni Pauni Milioni 60, lakini United inapambana kushusha dau. Wamekutana kwa mara ya pili na viongozi wa klabu hiyo ya Lisbon, baada ya kumuona Sanches katika mechi tatu zilizopita za klabu yake hiyo.
    Benfica imeweka bei kubwa kumuuz kinda huyo, lakini inatarajiwa kumuuza kwa nusu ya dau la Pauni Milioni 60 inazotaja.
    Manchester United inataka kumsajili Renato Sanches (katikati kushoto) kabla ya kufungwa kwa dirisha dogo mwezi huu PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YAKARIBIA KUINASA SAINI YA 'MIDO HATARI' LA BENFICA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top