• HABARI MPYA

    Sunday, January 31, 2016

    16 BORA KOMBE LA FA ENGLAND, MAN UNITED WAPEWA VIBONDE, CHELSEA NA MAN CITY, ARSENAL...

    Kocha wa Man United, Louis Van Gaal
    TIMU ya Chelsea imepangwa kumenyana na Manchester City katika Raundi ya Tano ya Kombe la FA Cup baada ya kuitoa MK Dons.  
    Manchester United wamepangiwa timu ya Daraja la Kwanza, Shrewsbury Town, wakati Arsenal walioshinda Kombe la FA misimu miwili mfululizo iliyopita watamenyana na Hull City, timu ambayo waliifunga kutwaa taji hilo mwaka 2014.  
    Liverpool na West Ham wanatarajiwa kumenyana katika mchezo wa marudiano baada ya sare ya 0-0 Uwanja wa Anfield Jumamosi na mshindi ataifuata na Blackburn Rovers.
    Tottenham itakuwa mwenyeji wa Crystal Palace Uwanja wa White Hart Lane, Reading itamenyana na mshindi wa mechi ya marudiano kati ya West Brom na Peterborough wakati Leeds itasafiri kuwafuata Watford na Bournemouth itamenyana na Everton Uwanja wa Vitality.  

    RATIBA KAMILI HATUA YA 16 BORA KOMBE LA FA ENGLAND: 

    Chelsea vs Manchester City
    Reading vs West Brom/Peterborough
    Watford vs Leeds
    Shrewsbury vs Manchester United
    Blackburn vs Liverpool/West Ham
    Tottenham vs Crystal Palace
    Arsenal vs Hull
    Bournemouth vs Everton
    (Mechi zitachezwa wikiendi ya Februari 19) 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: 16 BORA KOMBE LA FA ENGLAND, MAN UNITED WAPEWA VIBONDE, CHELSEA NA MAN CITY, ARSENAL... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top