TIMU ya Singida Black Stars imeichapa Tanzania Prisons mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na kiungo mshambuliaji Ayoub Reuben Lyanga dakika ya sita na beki Mghana, Ibrahim Imoro dakika ya 90’+1, wakati bao pekee la Tanzania Prisons limefungwa na mshambuliaji George Mpole kwa penalti dakika ya nne.
Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 25 katika mchezo wa 15 ikisogea nafasi ya tano, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake 13 za mechi 17 nafasi ya 15 kwenye Ligi ya timu 16.
Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.



.png)
0 comments:
Post a Comment