ORODHA YA MABINGWA KOMBE LA MAPINDUZI
Mwaka Bingwa Mshindi wa Pili
2007 Yanga SC Mtibwa Sugar
2008 Simba SC Mtibwa Sugar
2009 Miembeni KMKM
2010 Mtibwa Sugar Ocean View
2011 Simba SC Yanga SC
2012 Azam FC Simba SC
2013 Azam FC Tusker FC
2014 KCCA Simba SC
2015 Simba SC Mtibwa Sugar
Na Prince Akbar, ZANZIBAR
KIUNGO tegemeo wa Mtibwa Sugar, Shizza Kichuya amesema kwamba wapinzani wao URA katika fainali ya Kombe la Mapinduzi ni wazuri, lakini watapigana kiume kuhakikisha wanabakisha taji hilo nyumbani.
Kichuya anayeng’ara na Mtibwa Sugar katika michuano hii, kiasi cha kuzitamanisha timu kadhaa zikiwemo Azam, Simba na Yanga amesema kwamba mchezo wa kesho utakuwa mgumu, lakini watapambana kwa uwezo wao wote ili washinde.
“Tunafahamu kwa sasa matumaini ya Watanzania yapo kwetu sisi ili tuweze kubakisha Kombe hili nyumbani, baada ya ndugu zetu wote kutolewa. Na kwa kutambua hilo, sisi kama wachezaji tutajituma,”amesema.
Mtibwa Sugar inakutana na URA ya Uganda katika Fainali ya Kombe la Mapinduzi kesho usiku Uwanja wa Amaan, Zanzibar baada ya kuwatoa waliokuwa mabingwa watetezi, Simba SC Jumapili kwa kuwafunga 1-0.
URA imefika katika mechi ya mwisho ya Kombe la Mapinduzi, baada ya kuwatoa mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga SC kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 90.
Hii itakuwa mara ya tano kwa Mtibwa Sugar kufika fainali, baada ya awali kucheza fainali nne na kutwaa taji mara moja, 2010 ilipoifunga Ocean View ya hapa.
Mtibwa iliingia fainali mwaka 2007 na kufungwa na Yanga SC – wakati 2008 na 2015 ilifungwa na Simba SC mara zote.
URA ambao wanacheza mashindano haya kwa mara ya pili, hawajawahi kufika fainali, lakini mwaka 2014 taji la Mapinduzi lilipanda ndege kwenda Uganda, lilipochukuliwa na KCCA walioifunga Simba SC katika fainali.
Mwaka Bingwa Mshindi wa Pili
2007 Yanga SC Mtibwa Sugar
2008 Simba SC Mtibwa Sugar
2009 Miembeni KMKM
2010 Mtibwa Sugar Ocean View
2011 Simba SC Yanga SC
2012 Azam FC Simba SC
2013 Azam FC Tusker FC
2014 KCCA Simba SC
2015 Simba SC Mtibwa Sugar
Kiungo tegemeo wa Mtibwa Sugar, Shizza KIchuya amesema watapigana kiume kesho wabakishe Kombe nyumbani |
Na Prince Akbar, ZANZIBAR
KIUNGO tegemeo wa Mtibwa Sugar, Shizza Kichuya amesema kwamba wapinzani wao URA katika fainali ya Kombe la Mapinduzi ni wazuri, lakini watapigana kiume kuhakikisha wanabakisha taji hilo nyumbani.
Kichuya anayeng’ara na Mtibwa Sugar katika michuano hii, kiasi cha kuzitamanisha timu kadhaa zikiwemo Azam, Simba na Yanga amesema kwamba mchezo wa kesho utakuwa mgumu, lakini watapambana kwa uwezo wao wote ili washinde.
“Tunafahamu kwa sasa matumaini ya Watanzania yapo kwetu sisi ili tuweze kubakisha Kombe hili nyumbani, baada ya ndugu zetu wote kutolewa. Na kwa kutambua hilo, sisi kama wachezaji tutajituma,”amesema.
Mtibwa Sugar inakutana na URA ya Uganda katika Fainali ya Kombe la Mapinduzi kesho usiku Uwanja wa Amaan, Zanzibar baada ya kuwatoa waliokuwa mabingwa watetezi, Simba SC Jumapili kwa kuwafunga 1-0.
URA imefika katika mechi ya mwisho ya Kombe la Mapinduzi, baada ya kuwatoa mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga SC kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 90.
Hii itakuwa mara ya tano kwa Mtibwa Sugar kufika fainali, baada ya awali kucheza fainali nne na kutwaa taji mara moja, 2010 ilipoifunga Ocean View ya hapa.
Mtibwa iliingia fainali mwaka 2007 na kufungwa na Yanga SC – wakati 2008 na 2015 ilifungwa na Simba SC mara zote.
URA ambao wanacheza mashindano haya kwa mara ya pili, hawajawahi kufika fainali, lakini mwaka 2014 taji la Mapinduzi lilipanda ndege kwenda Uganda, lilipochukuliwa na KCCA walioifunga Simba SC katika fainali.
0 comments:
Post a Comment