• HABARI MPYA

    Friday, February 22, 2019

    CHELSEA YAICHAPA MALMO 3-0 NA KUSONGA MBELE EUROPA LEAGUE

    Mshambuliaji kinda wa England mwenye asili ya Ghana, Callum Hudson-Odoi mwenye umri wa miaka 18 akishangilia baada ya kuifungia Chelsea bao la tatu dakika ya 84 katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Malmo FF kwenye mchezo wa hatua ya 32 Bora UEFA Europa League usiku wa jana Uwanja wa Stamford Bridge mjini London. Mabao mengine ya Chelsea yamefungwa na Olivier Giroud dakika ya 55 na Ross Barkley dakika ya 74 na kwa matokeo hayo Chelsea inasonga mbele kwa ushindi wa 5-1, kufuatia kushinda 2-1 kwenye mchezo wa kwanza pia nchini Sweden  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA YAICHAPA MALMO 3-0 NA KUSONGA MBELE EUROPA LEAGUE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top