• HABARI MPYA

    Thursday, February 28, 2019

    SUAREZ APIGA MBILI BARCELONA YAICHAPA REAL MADRID 3-0

    Luis Suarez akiwa amezingirwa na wachezaji wenzake akiwemo, Lionel Messi wakimpongeza baada ya kufunga mabao mawili dakika za 50 na 73 kwa penalti katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Real Madrid lingine Raphael Varane akijifunga dakika ya 69 kwenye mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali ya Kombe la Mfalme Hispania usiku wa jana Uwanja wa Bernabeu. Barcelona inatinga fainali kwa ushindi wa jumla wa 4-1 baada ya sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Camp Nou Februari 6, mwaka huu na sasa itakutana na mshindi wa jumla kati ya Real Betis na Valencia zinazokutana usiku wa leo baada ya kutoa sare ya 2-2 kwenye mechi ya kwanza 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUAREZ APIGA MBILI BARCELONA YAICHAPA REAL MADRID 3-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top