• HABARI MPYA

    Saturday, August 20, 2016

    BOCCO AINUSURU AZAM FC KULALA KWA AFRICAN LYON CHAMAZI, SARE 1-1

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    BAO la Nahodha John Raphael Bocco dakika ya 93 usiku huu limeinusuru Azam FC kulala mbele ya African Lyon baada ya kupata sare ya 1-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Bocco alifunga bao hilo lililokuwa likisubiriwa kwa hamu akimalizia pasi nzuri ya kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
    Lyon walitangulia kwa bao lililofungwa na Mganda Hood Abdul Mayanja dakika ya 46 baada ya kuchonga kona iliyoingia moja kwa moja nyavuni.
    Sifa zimuendee kipa wa Lyon, Youthe Rostand aliyeokoa michomo mingi leo na ya hatari kabla ya kukubali bao la dakika ya 93.
    Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Ismail Gambo/Mudathir Yahya dk46, Bruce Kangwa, Himid Mao, David Mwantika, Jean Mugiraneza, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Francesco Zekumbariwa dk64, Shomary Kapombe, Frank Domayo/Kipre Balou dk63, John Bocco na Shaaban Idd.
    Afrcan Lyon; Youthe Rostand, Baraka Jaffar, Khalfan Twenye, Hamad Waziri, William Otone, Omar Salum, Hamad Manzi, Mussa Nampaka, Omar Abdallah/Abdul Hilal dk86, Hood Mayanja na Tito Okello.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BOCCO AINUSURU AZAM FC KULALA KWA AFRICAN LYON CHAMAZI, SARE 1-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top