• HABARI MPYA

    Monday, August 22, 2016

    WAZIRI NAPE AKABIDHIWA SHAMBA LA BIBI, LIGI KUU BYE- BYE TAIFA

    Na Khalfan Said, DAR ES SALAAM
    SERIKALI imekabidhiwa rasmi uwanja wa Taifa wa Uhuru, (pichani juu), jijini Dar es Salaam, leo Agosti 22, 2016, baada ya ukarabati mkubwa wa uwanja huo kukamilika.
    Akipokea uwanja huo kwa niaba ya Serikali, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amewapongeza wakandarasi ambao ni kampuni ya China ya Beijing Construction Engineering Group Company Limited, (BCEG), na mshauri mwelekezi wa uwanja huo kampuni ya kizalendo chini ya uongozi wa ke, Injinia Aloyce Peter Mushi kwa kazi nzuri iliyofanyika licha ya mikwamo ya hapa na pale.
    “Ndugu zetu Wachina, wameonyesha sio tu uhusiano mzuri bali wameonyesha kuwa wao ni ndugu zetu, kwani walishiriki wakati nchi yetu ikipata uhuru laini toka wakati huo hadi hivi sasa, bado wanashiriki katika kusaidia kuimarisha uchumi wetu,” alisema.
    Mwonekano wa Uwanja wa Uhuru baada ya ukarabati mkubwa PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    Waziri Nanuye aliwataka watumiaji wa uwanja huo kulipa ada za matumizi kama inavyostahili, ili hatimaye fedha hizo ziweze kugharimia matunzo ya uwanja.
    Akitoa taarifa ya ujezni huo, mshauri huyo mwelekezi wa ujenzi, Injinia Aloyce Peter Mushi alisema, uwanja huo una uwezo wa kuchukua watu milioni 22 na ulikamilika na kuanza kutumika kwa mara ya kwanza Mei 22, 2015.
    Naye Meneja Mkuu wa Kampuni ya BCAG, Cheng Long Hai, alisema, uwanja huo umewekewa mifumo yote muhimu kama vile tangi la kuhifadhia maji na mifumo ya maji taka, na kuishukuru serikaliya Tanzania kwa kuiaminikampuni yake kutekeleza mradi huo mkubwa.
    Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, alisema, amekuwa akipokea maombi mbalimbali ya wanamichezo na watu wengine kuomba kuutumia uwanja huo na kuwahakikishia kuwa utaratibu unapangwa ili watanzania waanze kufaidi matunda ya uwanja huo ambao kutokana na ukongwe wake ulipachikwa jina la shamba la bibi.
    “Nitoe rai tu kwa watanzania, leohii Agosti 22, 2016 ambapo tumekabidhiwa uwanja huu rasmi ukiwa umekamilika, naomba hilo jina la shambala bibi nalo lifikie kikomo kwani uwanja huu sa sa unauonekano mpya na wa kisasa.” Alisema Profesa Gabriel.
    Ukarabati huo mkubwa ulihusisha ujenzi wa jukwaa na paa, ikiwa ni pamoja na miundombinu mingine ya uwanja kama vile, mifumo ya kusambaza maji, na kutoa maji taka, uwekani wa tanki la kuhifadhia maji, pamoja na ujenzi wa vyoo vya kutosha uwanjani.
    Baada ya Serikali kukabidhiwa Uwanja wa Uhuru sasa mechi zote za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kuanzia wikiendi hii zinahama Uwanja wa Taifa.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAZIRI NAPE AKABIDHIWA SHAMBA LA BIBI, LIGI KUU BYE- BYE TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top