• HABARI MPYA

    Saturday, August 13, 2016

    BAO LA YANGA LILIVYOPATIKANA NA ALIYEFUNGA HADI MTOA PASI

    Winga wa Yanga, Simon Msuva akipiga kichwa kuelekeza langoni mwa MO Bejaia baada ya krosi ya beki wa kulia, Juma Abdul (hayupo pichani) katika mchezo wa Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga ilishinda 1-0
    Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe akiunganisha mpira wa Msuva kuifungia Yanga bao pekee la ushindi kwenye mchezo huo
    Tambwe alifanikiwa kuwazidi mabeki watatu na kipa wa MO Bejaia na kuutunbukiza mpira nyavuni
    Pamoja na mpira kuvuka mstari, lakini mchezaji mmoja wa MO Bejaia aliurudisha uwanjani 
    Tambwe alipambana sana kwenye lango la MO Bejaia
    Na baada ya kujiridhisha amefunga, akageuka kwenda kushangilia bao lake
    Mabeki wa MO Bejaia walitaka kumdanganya refa, lakini hawakufanikiwa na bao hilo lilikubaliwa 
    Hapa Tambwe ananyoosha mkono kumpinga mshika kibendera aliyekataa bao hilo, lakii refa alikubali bao na Yanga imeshinda 1-0
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BAO LA YANGA LILIVYOPATIKANA NA ALIYEFUNGA HADI MTOA PASI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top