• HABARI MPYA

    Saturday, August 13, 2016

    MESSI ABATILISHA UAMUZI WA KUSTAAFU KUICHEZEA ARGENTINA

    Lionel Messi alitangaza kustaafu soka ya kimataifa kwa sababu ya kufungwa fainali ya Copa America PICHA ZAIDI GONGA HAPA 


    REKODI ZA MESSI 

    NA ARGENTINA

    Jumla ya mechi: 11aa3 Mabao: 55
    Mechi ya kwnza: Agosti 17 2005, vs Hungary in Budapest (Argentina ilishinda 2-1)Bao la kwanza March 1 2006, vs Croatia mjini Basel, Uswisi(Argentina ilifungwa 3-2) 
    Vipigo vya kukumbukwa: 
    Copa America 2007, vs Brazil 0-3
    World Cup 2014, vs Ujerumani 0-1
    Copa America 2015 vs Chile 0-0 (walifungwa 4-1 kwa penalti)
    Copa America 2016 vs Chile 0-0 (walifungwa 4-2 kwa penalti)
    MWANASOKA bora wa dunia, Lionel Messi amebadilisha uamuzi wake wa kustaafu soka ya kimataifa na kurejea kuendelea kuichezea timu yake ya taifa, tena akisema anaipenda ile mbaya Argentina.
    Nyota huyo wa Barcelona alitangaza kustaafu soka ya kimataifa mara tu baada kukosa penalti katika fainali ya Copa America dhidi ya Chile mwezi Juni, Argentina wakifungwa.
    Pamoja na hayo, baada ya kukutana na kocha mpya wa timu ya taifa, Edgardo Bauza, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 amethibitisha kurejea kikosini.
    Messi, Nahodha wa Argentina na mfungaji bora wa kihistoria wa timu yake hiyo ya taifa kwa mabao yake 55, amesema katika taarifa yake amesema iliyochapishwa na gazeti la La Nacion: "Naona kuna matatizo mengi katika soka ya Argentina na sitaki kuongeza lingine moja. Sitaki kusababisha dosari yoyote,"alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI ABATILISHA UAMUZI WA KUSTAAFU KUICHEZEA ARGENTINA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top