• HABARI MPYA

    Thursday, March 17, 2016

    ARSENAL YAFA 'KISHUJAA' CAMP NOU

    Mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez akiunganisha kwa ustadi mkubwa krosi ya Dani Alves kuifungia timu yake bao la pili dakika ya 65 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Arsenal usiku huu Uwanja wa Camp Nou katika mchezo wa marudiano wa hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mabao mengine ya Barcelona yamefungwa na Neymar Junior dakika ya 18 na Lionel Messi dakika ya 88, wakati bao pekee la Arsenal limefungwa na Mohamed Elneny dakika ya 51. Barcelona inatinga Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa 5-1 baada ya awali kushinda 2-0 Uwanja wa Emirates, London PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YAFA 'KISHUJAA' CAMP NOU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top