• HABARI MPYA

    Sunday, March 20, 2016

    WADADA WATOLEWA KISHUJAA ZIMBABWE

    Twiga Stars imetolewa na Zimbabwe
    TIMU ya taifa ya soka ya wanawake Tanzania, Twiga Stars imetolewa katika mbio za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika licha ya kulazimisha sare ya 1-1 dhidi ya wenyeji, Zimbabwe ‘Mighty Warriors’ jioni ya leo katika mchezo wa mchujo wa marudiano Uwanja wa Rufaro mjini Harare.
    Zimbabwe inasonga mbele kwa ushindi wa ushindi wa 3-2, baada ya awali kushinda 2-1 mjini Dar es Salaam wiki iliyopita.
    Twiga inayozikosa Fainali za mwakani Cameroon, inatarajiwa kurejea nyumbani kesho mchana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WADADA WATOLEWA KISHUJAA ZIMBABWE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top