• HABARI MPYA

    Monday, March 21, 2016

    AZAM NA BIDVEST KATIKA PICHA CHAMAZI

    Mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Tchetche (kulia) akimchambua kipa wa Bidvest Wits ya Afrika Kusini kufunga moja ya mabao yake matatu katika ushindi wa 4-3 jana kwenye mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza Kombe la Shirikisho Afrika uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam jana. Azam imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 7-3 baada ya awali kushinda 3-0 Johannesburg wiki iliyopita
    Nahodha wa Azam FC, John Bocco akipambana katikati ya wachezaji wa Bidvest Wits
    Kiungo wa Azam FC, Jean Baptiste Mugiraneza akizuia mpira mbele ya mchezaji wa Bidvest
    Mchezaji wa Bidvest Wits akimiliki mpira mbele ya mshambuliaji wa Azam, John Bocco
    Kipre Tchetche (kushoto) akitafuta maarifa ya kumpita beki wa Bidvest
    Mshambuliaji wa Azam, Allan Wanga (kulia) akitafuta maarifa ya kumpita beki wa Bidvest Wits
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM NA BIDVEST KATIKA PICHA CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top