• HABARI MPYA

    Friday, April 17, 2026

    AZAM FC YAICHAPA JKT TANZANIA 3-0 CHAMAZI


    TIMU ya Azam FC imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiki hui Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Mabao ya Azam FC yamefungwa na mshambuliaji kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Jephte Kitambala Bola dakika ya 48 na winga Iddi Suleiman Ally ‘Nado’ mawili dakika ya 56 na 60.
    Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 37, ingawa inabaki nafasi ya tatu, ikizizidi pointi nane zote, JKT Tanzania na Singida Black Stars baada ya timu zote tatu kucheza mechi 19. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAICHAPA JKT TANZANIA 3-0 CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top