Kikosi cha Yanga SC kabla ya mchezo wake wa kwanza wa Robo ya Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika Kundi B dhidi ya ASEC Mimosa ya Ivory Coast Novemba 8, mwaka 1998 Uwanja wa Taifa (sasa Uhuru) mjini Dar es Salaam uliomalizika kwa wageni kushinda 3-0. Kutoka kulia waliosimama ni Salvatory Edward, Banza Tshikala, Edibily Lunyamila, Manyika Peter, Idelphonce Amlima na Alphonce Modest. Waliochuchumaa kutoka kulia ni Monja Liseki, Mohammed Hussein ‘Mmachinga’, Shaaban Ramadhani, Mzee Abdallah ‘National’ na John Jacob Mwansasu. Yanga SC walilazimika kuvaa jezi za Taifa Stars kutokana na jezi zao pekee walizokuwa nazo (njano) kufanana na za wageni.
CHRIS SUTTON: The United job was supposedly 'too big' for Solskjaer but he's proving people wrong
-
CHRIS SUTTON: Bruno Fernandes was told he wouldn't start against Liverpool.
But the day before the game, he stayed behind after training and practised
taki...
38 minutes ago
0 comments:
Post a Comment