TIMU ya Azam FC imelazimisha sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji, Pamba Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
Ni Pamba Jiji waliouanza vyema mchezo huo na kupata mabao mawili ya uongozi kupitia kwa kiungo wa Azam FC, Himid Mao Mkami aliyejifunga dakika ya 45 na mshambuliaji wake, Mganda John Ben Nakibinge dakika ya 48.
Lakini Azam FC ikazinduka kipindi cha pili na kusawazisha mabao yote kupitia kwa mshambuliaji Mkongo, Jean-Jacques Ngita dakika ya 56 na kiungo Feisal Salum Abdallah kwa penalti dakika ya 59, kabla ya kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 62.
Kwa matokeo hayo, Azam FC inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 11, ingawa inabaki nafasi ya tano ikizidiwa pointi moja na Pamba Jiji FC ambayo pia imecheza mechi nne zaidi.



.png)
0 comments:
Post a Comment