• HABARI MPYA

    Monday, March 02, 2026

    PAMBA NA AZAM FC NGOMA DROO MWANZA, ZAFUNGANA 2-2 CCM KIRUMBA


    TIMU ya Azam FC imelazimisha sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji, Pamba Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
    Ni Pamba Jiji waliouanza vyema mchezo huo na kupata mabao mawili ya uongozi kupitia kwa kiungo wa Azam FC, Himid Mao Mkami aliyejifunga dakika ya 45 na mshambuliaji wake, Mganda John Ben Nakibinge dakika ya 48.
    Lakini Azam FC ikazinduka kipindi cha pili na kusawazisha mabao yote kupitia kwa mshambuliaji Mkongo, Jean-Jacques Ngita dakika ya 56 na kiungo Feisal Salum Abdallah kwa penalti dakika ya 59, kabla ya kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 62.
    Kwa matokeo hayo, Azam FC inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 11, ingawa inabaki nafasi ya tano ikizidiwa pointi moja na Pamba Jiji FC ambayo pia imecheza mechi nne zaidi.


    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PAMBA NA AZAM FC NGOMA DROO MWANZA, ZAFUNGANA 2-2 CCM KIRUMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top