• HABARI MPYA

    Tuesday, March 15, 2016

    TFF YAREKEBISHA TENA RATIBA LIGI KUU

    RATIBA MPYA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA;
    Machi 16, 2016
    Azam FC Vs Stand United
    Machi 18, 2016
    Kagera Sugar Vs Mtibwa Sugar
    Machi 19, 2016
    Coastal Union Vs Simba SC
    Majimaji Vs Mbeya City
    Stand United Vs Ndanda FC
    Machi 20, 2016
    African Sports Vs Prisons
    Machi 21, 2016
    Mgambo JKT Vs Toto Africans
    Machi 24, 2016
    African Sports Vs Toto Africans
    Aprili 2, 2016
    Majimaji Vs Simba SC
    Yanga SC Vs Kagera Sugar
    Toto Africans Vs Azam FC
    Stand United Vs Mgambo JKT
    Ndanda FC Vs Prisons
    Mbeya City Vs Coastal Union
    Aprili 3, 2016
    JKT Ruvu Vs African Sports
    Mwadui FC Vs Mtibwa Sugar
    Aprili 5, 2016
    Toto Africans Vs Yanga SC
    Azam FC Vs Ndanda FC
    Aprili 9, 2016
    Stand United Vs Yanga SC
    Ndanda FC Vs Mwadui FC
    Na Somoe Ng’itu, DAR ES SALAAM
    YANGA haitacheza mechi yoyote ya Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara mwezi huu, wakati wapinzani wao katika mbio za ubingwa, Simba na Azam watacheza mechi moja moja.
    Kwa mujibu wa marekebisho ya Ratiba ya Ligi Kuu yaliyotolewa leo, Azam FC watacheza na Stand United kesho Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, wakati Simba SC watacheza na Coastal Union Jumamosi Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. 
    Bodi ya Ligi imelazimika kufanya marekebisho ya Ratiba ya Ligi Kuu kupisha ratiba ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars katika mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika 2017.
    Taifa Stars itakuwa na mchezo wa kufuzu AFCON Kundi G dhidi ya Chad mjini N’jamena Machi 25, kabla ya timu hizo kurudiana Machi 28, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Na baada ya mechi za mwishoni mwa wiki za michuano ya klabu barani, Afrika wachezaji wa Stars wanatarajiwa kukusanywa Jumapili kabla ya safari Jumanne kuelekea Chad.
    Yanga SC baada ya ushindi wa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya APR Jumamosi mjini Kigali, watarudiana na timu hiyo ya jeshi la Rwanda Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Na Azam FC baada ya kushinda 3-0 mjini Johannesburg, Afrika Kusini dhidi ya wenyeji Bidvest Wits katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Kombe la Shirikisho Afrika, watarudiana na timu hiyo Jumapili, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Ligi Kuu itaendelea Aprili 2, kwa Yanga kumenyana na Kagera Sugar Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Simba SC kumenyana na Majimaji Uwanja wa Majimaji mjini Songea, wakati Azam FC watakuwa wageni wa Toto Africans Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF YAREKEBISHA TENA RATIBA LIGI KUU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top