MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji, Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
Bao pekee la Yanga SC leo limefungwa na mshambuliaji mpya, Laurindo Dilson Maria Aurélio 'Depu' aliyesajiliwa dirisha dogo kutoka Radomiak S.A., inayofahamika zaidi kama Radomiak Radom ya Poland kwa penalti dakika ya 26.
Kwa ushindi huo, Yanga SC inafikisha pointi 25 katika mchezo wa tisa na kusogea nafasi ya pili ikizidiwa pointi tatu na JKT Tanzania ambayo pia imecheza mechi 16.
Kwa upande wao, Namungo FC baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki na poinyi zao 20 za mechi 15 sasa nafasi ya tano.



.png)
0 comments:
Post a Comment