• HABARI MPYA

    Saturday, February 14, 2026

    TANZANIA imeitoa Kenya katika mbio za kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake chini ya umri wa miaka 20 kufuzu Fainali za Kombe la Dunia kwa penalti 3-1 kufuatia sare ya jumla ya 1-1 kila timu ikishinda 1-0 nyumbani katika Raundi ya Tatu.
    Mchezo Februari 7 Kenya ilishinda 1-0 Uwanja wa Ulinzi Sports Complex, Nairobi na katika marudiano Tanzania nayo imeshinda 1-0 jioni ya leo Uwanja Wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Hata hivyo, Tanzania ikafanikiwa kwenda Raundi ya Nne na ya mwisho ya mchujo huo kwa ushindi Wa penalti 3-1 na sasa itakutana na Cameroon mwezi Mei katika mechi nyingine mbili za nyumbani na ugenini.
    Timu nne zitaiwakilisha Afrika katika Fainali za Kombe la Dunia la FIFA U20 Wanawake 2026 U-20 nchini Poland.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top