TIMU ya Singida Black Stars imefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Mbeya City Uwanja wa Airtel Mwigulu mjini Singida.
Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na Khalid Aucho, winga wa kulia Mgambia, Lamin Jarjou, beki wa kushoto Mghana Ibrahim Imoro mawili na mshambuliajii kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Malanga Horso Mwaku.



.png)
0 comments:
Post a Comment