![]() |
| Mshambuliaji Mkenya, Elvis Baranga Rupia akishangilia baada ya kuifungia Singida Black Stars bao la kuongoza |
TIMU ya Namungo FC imetoa sare ya kufungana bao 1-1 na Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
Mkenya, Elvis Baranga Rupia alianza kuifungia Singida Black Stars dakika ya 58 kwa penalti, kabla ya mshambuliaji mwenzake, Mkongo - Fabrice Ngoy wa Ngoy kuisawazishia Namungo FC dakika ya 90’+1.
Kwa matokeo hayo, Namungo FC inafikisha pointi 21 katika mchezo wa 16 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya sita, wakati Singida Black Stars inafikisha pointi 16 katika mchezo wa 10 na kupanda kwa nafasi mbili pia hadi ya 10.



.png)
0 comments:
Post a Comment