• HABARI MPYA

    Monday, August 21, 2017

    TFF YAMZUIA CHIRWA KUICHEZEA YANGA DHIDI YA SIMBA JUMATANO TAIFA

    Na Rehema Lucas, DAR ES SALAAM
    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limemzuia kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mzambia Obrey Chirwa kucheza mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Jumatano.
    Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas amesema leo katika mkutano na Waandishi wa Habari mjini Dar es Salaam kwamba, Chirwa hawezi kucheza kesho kwa sababu katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Mbao FC alimsukuma refa mjini Mwanza.
    “Chirwa atakukosa mchezo wa Jumatano dhidi ya Simba utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa saa 11:00 mjini Dar es Salaam kutokana na kesi inayomkabili ya kumsukuma mwamuzi aliyechezesha mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu dhidi ya Mbao FC,”alisema.
    TFF imemzuia Mzambia Obrey Chirwa kucheza Yanga dhidi ya Simba SC Jumatano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

    Lucas amesema mshambuliaji aliyejiunga na Yanga msimu uliopita kutoka PF Platinums ya Zimbabwe amesema atalazimika kuendelea kuwa nje hadi hapo Kamati ya Masaa 72 itakapokutana na kutoa maamuzi dhidi yake.
    Pamoja na Chirwa, ambaye hata hivyo ni majeruhi na hayupo kambini kisiwani Pemba, wengine watakoukosa mchezo huo upande wa Yanga ni maheruhi ni kipa Beno Kakolanya na kiungo Goffrey  Mwashiuya.
    Lucas amewataja marefa watakaochezesha mechi hiyo ni Elly Sasii kutoka Dar es Salaam, atakayesaidiwa na Ferdinand Chacha na Hellen Mduma.
    Viingilio katika mchezo huo ni Sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya kijani na bluu, 10,000 Viti vya Orange, 20,000 kwa VIP B ba 25 kwa VIP A .
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF YAMZUIA CHIRWA KUICHEZEA YANGA DHIDI YA SIMBA JUMATANO TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top