• HABARI MPYA

    Wednesday, August 30, 2017

    APR YAMSAJILI MCHEZAJI ALIYEGOMA KUCHEZA BURE HISPANIA

    Na Canisius Kagabo, KIGALI
    KLABU ya APR FC ya Rwanda, imemsajili beki chipukizi wa kulia Ombalenga Fitina (pichani kushoto) baada ya mipango yake ya kucheza Hispania kugonga besela.
    Fitina alikaribia kujiunga na klabu ya Ligi Daraja la Kwanza Hispania, Universidad Catolica de Murcia (UCAM Murcia) baada ya kufuzu majaribio yeye pamoja na chipukizi mwenzake wa Rwanda, Kalisa Rashid.
    Lakini wote akaamua kurudi nyumbani, baada ya kuambiwa anapaswa kwanza kucheza kikosi cha vijana cha timu hiyo kwa miezi sita kama mchezaji wa ridhaa, kabla ya kupewa mkatava rasmi, ingawa mwenzake Kalisa Rashid bado hajasaini timu yeyote.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: APR YAMSAJILI MCHEZAJI ALIYEGOMA KUCHEZA BURE HISPANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top