• HABARI MPYA

    Thursday, August 24, 2017

    LIVERPOOL YAZIFUATA MAN CITY, UNITED MAKUNDI LIGI YA MABINGWA

    Emre Can akishangilia baada ya kuifungia mabao mawili Liverpool jana dakika za 10 na 21 ikishinda 4-2 Uwanja wa Anfield dhidi ya Hoffenheim ya Ujerumani katika mchezo wa marudiano wa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. 
    Mabao mengine ya Liverpool yalifungwa na Mohamed Salah dakika ya 18 na Roberto Firmino dakika ya 63, wakati ya Hoffenheim yamefungwa na Mark Uth dakika ya 28 na Sandro Wagner dakika ya 79. 
    Liverpool inakwenda hatua ya makundi kwa ushindi wa jumla wa 6-3 baada ya awali kushinda 2-1 Ujerumani. Inaungana na timu nyingine za England, Chelsea, Manchester City, Manchester United na Tottenham Hotspur PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YAZIFUATA MAN CITY, UNITED MAKUNDI LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top